Rafiki Credit Service® ni mdau wako katika sekta ya fedha. Lengo letu ni kuleta mabadiliko chanya katika jamii yetu kwa kusaidia wajasiriamali wadogo na watu wengine wa kipato cha chini kupata mikopo yenye riba nafuu na masharti himilivu ili kuimarisha biashara zao na kutatua changamoto mbali mbali za kimaisha. Tunaamini kwamba kwa kufanya hivyo, tutachangia katika kupunguza umaskini na kukuza maendeleo ya wajasiria mali na taifa kwa ujumla.
Inafahamika kwamba wajasiriamali wengi na watu wa kipato cha chini wana changamoto kubwa kufikia huduma za kifedha katika benki na taasisi kubwa zinazotoa huduma za mikopo. Rafiki Credit Service® inalenga kuziba pengo hili kwa kuwapa fursa mbadala wahitaji wote wa mikopo midogo midogo.
Tunatoa Mikopo ya Dharura na Biashara kwa dhamana ya mali na vifaa vidogo vidogo kama vile simu, TV, feni, redio, subwoofer na vingine kama hivyo. Riba zetu ni himilivu na nafuu sana na mikopo hutolewa kwa kipindi cha mwezi mmoja mpaka miwili.
WASILIANA NASI (+255) 763 94 94 94
Kuwa mojawapo ya taasisi zitakazoongeza chachu ya mabadiliko katika kuweza watu wote kupata huduma za kifedha na mikopo na kuwasaidia wahitaji kufikia malengo yao kijamii na kiuchumi kwa kupata mikopo nafuu yenye Riba himilivu.
Tunadhamiria kuwezesha watu wa kipato cha chini na wajasiria mali wadogo kupata kimbilio la hitaji la mikopo midogo ili kupambana na changamoto za mtaji na dharura za kibiashara na kijamii.
Kuongeza ubunifu katika utoaji huduma wenye kulinda na kuheshimu 'utu' wa mteja. Watendaji wa Rafiki Credit Service® wanachagizwa kutoa huduma kwa kulinda 'utu' na heshima ya mteja.
Rafiki Credit Service® inatoa huduma ya mikopo pamoja na huduma nyingine za Uwakala wa Fedha, Uandishi wa Mpango Biashara na uwakala wa Mifumo ya Tehama
Tunatoa huduma mbali mbali za Uwakala wa Benki na Simu
Tunatoa huduma ya Utaalamu na Uandishi wa Mpango Biashara
Tunatoa huduma ya usambazaji wa Mifumo ya kidijitali (software) ya kuendesha Biashara & Huduma
Ili kupata maelezo zaidi kuhusu huduma zetu, tafadhali tembelea mitandao yetu ya kijamii, au wasiliana nasi kwa simu, au tembelea tawi letu lililo karibu.
Mikopo yetu hutolewa kwa dhamana ya mali na/au vitu vinavyohamishika kama vile:-
Laptop
TV
Subwoofer
Simu
iPad/Tablet
Kompyuta (Desk-top)
Ili kupata huduma ya Mkopo toka Rafiki Credit Service® unatakiwa kuwa na dhamana ya mali/kifaa kilichoidhinishwa kama vile simu, laptop n.k.
Utaratibu wetu ni rahisi sana na hauna mlolongo wa vigezo na masharti magumu.
Mikopo yetu ina Riba nafuu sana na himilivu kulinganisha na watoa huduma wengine.
Mkopo wa Miezi 2 Riba ni 30%
Mkopo wa Mwezi 1 Riba ni 20%
Kanuni ya Riba inayotumika ni Fixed Interest Method
Mfano: Mkopo wa Tsh 100,000/- Riba yake itakuwa Tsh 30,000/- kwa miezi 2 na Tsh 20,000/- kwa mwezi 1
Tunatoa Mkopo wa Nyongeza (Loan Top-up) kwa Mteja mwaminifu aliyetimiza masharti yafuatayo:-
Awe amerejesha angalau asilimia 50 ya Mkopo wa awali
Awe na historia nzuri ya kurejesha mikopo yake kwa wakati
Vigezo na Masharti kuzingatiwa
Tunaheshimu sana faragha ya wateja wetu. Taarifa yoyote inayojazwa kwenye fomu ya maombi ya Mkopo itatumika tu kwa ajili ya kumbu kumbu za Mkopo.
Kwa wateja waliokosa sifa za kupata Mkopo taarifa zao huaribiwa (disposed), mara moja.
Hatubadilishani taarifa za wateja wetu na shirika au kampuni yoyote